Waziri wa Nchi – Ofisi ya Rais – Fedha na Mipango Mhe Dkt Saada Mkuya Salum leo amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkaazi wa Benki ya Dunia Nchini Tanzania Ndg. Nathan Balete

Waziri wa Nchi – Ofisi ya Rais – Fedha na Mipango Mhe Dkt Saada Mkuya Salum leo amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkaazi wa Benki ya Dunia Nchini Tanzania Ndg. Nathan Balete mazungumzo hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Rais – Fedha na Mipango

Mhe Dkt. Saada akiwa na mgemi wake wamejadili kwa pamoja Miradi ya Maendeleo ambayo inafadhiliwa na benki ya Dunia ikiwemo miradi inayoendelea na Miradi ya vipao mbele vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ikiwemo miradi ya kuimarisha Nishati mbadala( ZEST)

Mradi wa kuimarisha miundombinu ya maji Unguja na Pemba, Mradi wa Elimu ambao unatekelezwa kwa pamoja na Tanzania bara mradi huu unalenga kuboresha mazingira ya kusomea kwa vyuo vikuu kwa kujengwa miundombinu mbalimbali

Aidha Dkt. Saada ameishukuru Benki ya Dunia kwa kuendelea kushirikiana na Zanzibar katika kuleta maendeleo ya haraka hapa nchini.

Mhe dkt. Saada amesema Mradi wa sekta ya Afya utasaidia kuboresha vituo vya afya nchini, na kujenga uwezo wa madaktari na madaktari bingwa sambamba na kutatua changamoto za mama wajawazito na watoto wakati wa kujifungua.

Mkurugenzi Nathan atakuwa na ziara ya siku mbili hapa Zanzibar akikagua Miradi iliyofadhiliwa na Benki ya Dunia

Imeandaliwa na Kitengo cha Habari na Uhusiano
Ofisi ya Rais – Fedha na Mipango

Serikali ya Jamhuri ya Korea Imeiwezesha Tanzania kupata Mikopo yenye Masharti nafuu kutoka Mfuko wa Ushirikiano wa Maendeleo ya Uchumi (EDCF).

Serikali ya Jamhuri ya Korea imeiwezesha Tanzania kupata mikopo yenye masharti nafuu kutoka Mfuko wa Ushirikiano wa Maendeleo ya Uchumi (EDCF) wa Korea yenye thamani ya Dola za Marekani bilioni moja ili kugharamia miradi ya maendeleo katika kipindi cha kuanzia mwaka 2021 hadi 2025.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Fedha na Mipango Zanzibar Mhe. Dkt. Saada Mkuya Salum, alieongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano kati ya Korea na Afrika (KOAFEC) kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, alipokutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Uchumi na Fedha wa Korea Mhe. Kyungho Choo, pembezoni mwa Mkutano kati KOAFEC unaoendelea jijini Busan nchini Korea Kusini.

Alisema kuwa mikopo hiyo kutoka Korea imesaidia utekelezaji wa miradi mbalimbali katika pande zote mbili za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na baadhi ya miradi iliyoidhinishiwa fedha mwezi Februari, 2023 ipo katika hatua mbalimbali za maandalizi.

‘Miradi iliyokatika hatua mbalimbali za utekelezaji ni pamoja na ujenzi wa hospitali ya rufaa ya Binguni inayotarajiwa kugharimu takriban dola za Marekani milioni 164, kuboresha hospitali ya Taifa ya Muhimbili dola milioni 227.3, ujenzi wa taasisi ya mafunzo dola milioni 75.8 na ujenzi wa taasisi ya teknolojia dola milioni 60, ujenzi wa kituo cha kisasa cha mafunzo ya reli dola milioni 75.8 na fedha nyingine zitaelekezwa katika sekta za nishati, uvuvi na fedha,’’alisema Mhe. Mkuya.

Alisema kuwa Tanzania ilipata mkopo wa masharti nafuu kutoka Mfuko wa Ushirikiano wa Maendeleo ya Uchumi (EDCF) kwa ajili ya ujenzi wa daraja la Selander (Tanzanite Bridge) uliogharimu Dola za Marekani milioni 123.65 ambapo daraja hilo si tu limebadilisha taswira ya jiji la Dar es Salaam, lakini pia limepunguza kwa kiasi kikubwa msongamano wa magari katika barabara ya Ali Hassan Mwinyi.

Aidha, Serikali ya Jamhuri ya Korea kupitia benki ya Exim ya Korea pamoja na Shirika la Bima la Korea (Ksure) imeendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kutekeleza mradi wa reli ya kisasa ya (SGR) ikihusisha utengenezaji wa vichwa na mabehewa ya treni.

‘‘Jumla ya fedha zilizotolewa na benki ya Exim na Ksure kwa ajili ya ununuzi wa vichwa na mabehewa ya treni yanayotengenezwa na Kampuni ya M/S Hyundai Rotem ya Jamhuri ya Korea ni dola za Marekani milioni 302.4”, alieleza Dkt. Mkuya.

Aidha katika mkutano huo, Mhe. Dkt. Mkuya aliiomba Serikali ya Jamhuri ya Korea kuharakisha mradi wa Ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Binguni na mradi wa Uendelezaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kutokana na umuhimu wa miradi hiyo katika kutoa huduma za Afya za kibingwa nchini Tanzania.

Akizungumza kuhusu uchumi wa Tanzania Mhe. Dkt. Mkuya alisema kuwa licha ya changamoto ya Covid 19 na vita ya Urusi na Ukraine Uchumi umeanza kuimarika katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2023 ambapo ukuaji uliorekodiwa ulikuwa wa asilimia 5.6 kwa Bara na ulikuwa asilimia 6.2 kwa Zanzibar.

Mhe. Dkt. Mkuya, aliishukuru Serikali ya Jamhuri ya Korea kwa kuendelea kuiunga mkono Tanzania, kutekeleza ajenda ya Maendeleo ya Taifa kama ilivyoainishwa chini ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2025, Dira ya Maendeleo ya Zanzibar 2050 na Mpango wa Tatu wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2021/22–2025/26 na Mpango wa Maendeleo wa Zanzibar 2021 -2026.

Alisisitiza kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, itaendelea kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Korea kwa ajili ya maendeleo ya watu wetu.

Kwa upande wake Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Uchumi na Fedha wa Korea Mhe. Kyungho Choo, alisema kuwa Korea itaendelea kushirikiana na Tanzania katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Imetolewa na
Kitengo cha Habari na Uhusiano
Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango
16 Sept, 2023

Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) inatarajia kusaidia utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Reli ya Kisasa kwa Kiwango cha Kimataifa (SGR).

Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) inatarajia kusaidia utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Reli ya Kisasa kwa Kiwango cha Kimataifa (SGR) kwa kipande cha Tabora – Kigoma (lot 6) na Uvinza – Malagarasi (lot 7) kwa takribani dola za Marekani bilioni 3.05 na kufadhili maandalizi ya mradi wa Ujenzi wa Bandari ya Mangapwani Zanzibar kwa takribani dola za Marekani milioni 60.

Hayo yameelezwa na Rais AfDB, Mhe. Dkt. Akinwumi Adesina, alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango – Zanzibar, Mhe. Dkt. Saada Mkuya, pembezoni mwa vikao vya mkutano wa saba wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea Kusini na Nchi za Afrika (KOAFEC), Mjini Busan, Jamhuri ya Korea Kusini.
“Benki ya Mandeleo ya Afrika inafanyia kazi upatikanaji wa kiasi cha dola za Marekani bilioni 3.05 kwa wakati ili kuwezesha kutekelezwa kwa mradi wa SGR kwa manufaa ya Tanzania pamoja na nchi za jirani”, alieleza Dkt. Adesina.
Akizungumzia kuhusu ushirikishwaji wa Sekta binafsi katika utekelezaji wa miradi, Dkt. Adesina alisema kuwa kuna umuhimu wa kuhusisha sekta hiyo katika utekelezaji wa miradi ya kimkakati nchini Tanzania ili kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kukuza uchumi.
Dkt. Adesina alisisitiza kuwa ni vyema kuendeleza sekta binafsi kwa kuwa ni muhimu katika kukuza uchumi kwa kasi na pia akaishauri Serikali kutumia fursa ya dirisha la AfDB (non- Sovereign Window) kwa ajili yakuimarisha na kuwezesha sekta binafsi nchini.

Aidha, alieleza kuwa Benki ya AfDB ipo tayari kuendelea kuisaidia Tanzania kupiga hatua kimaendeleo hasa katika miradi ya Kilimo, huku akiutaja mradi wa Kilimo wa Building Better Tomorrow (BBT) kuwa utatoa ajira kwa vijana wengi na kuongezeka kwa uzalishaji wa chakula nchini.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango – Zanzibar Mhe. Dkt. Saada Mkuya Salum, akiongoza ujumbe wa Tanzania kwa niaba ya Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), aliishukuru Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa kuongezea Tanzania mgao wa fedha kupitia dirisha la mikopo nafuu (ADB) kwa mwaka 2023 kutoka UA 160 milioni sawa na dola za Marekani milioni 216 hadi UA 560 milioni sawa na dola za Marekani milioni 756.

Dkt. Mkuya alieleza kuwa kutokana na umuhimu wa miradi ambayo AfDB imeonesha nia ya kuifadhili hususani mradi wa ujenzi wa bandari ya Mangapwani Zanzibar, ameiomba Benki hiyo ione namna ya kuweza kufanikisha upatikanaji wa fedha kwa ajili ya kutekeleza mradi huo kabla ya mwaka 2025.

‘’Tayari tumefanya upembuzi yakinifu katika mradi wa bandari ya Mwangapwani hivyo upatikanaji wa fedha utawezesha mradi huo kuanza mara moja”, alieleza Dkt. Mkuya.

Imetolewa na
Kitengo cha Habari na Uhusiano
Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango
15 Sept, 2023

MHE. DKT SAADA MKUYA SALUM AKIENDELEA KATIKA ZIARA NCHINI KOREA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Zanzibar, Mhe. Dkt. Saada Mkuya Salum, akichangia mada katika ajenda zilizolenga kuangalia namna nchi za Afrika zinaweza kuondokana na changamoto ya nishati pamoja na kuleta mageuzi ya kilimo barani Afrika, katika mkutano wa saba wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea Kusini na Nchi za Afrika (KOAFEC), Mjini Busan, Jamhuri ya Korea Kusini.

MHE. DKT SAADA MKUYA SALUM AKIWA KATIKA ZIARA NCHINI KOREA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Zanzibar, Mhe. Dkt. Saada Mkuya Salum, akizungumza na ujumbe wa Tanzania wakati wa kikao cha kukamilisha mapitio ya taarifa zitakazowasilishwa na Tanzania, katika mkutano wa saba wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea Kusini na Nchi za Afrika (KOAFEC), Mjini Busan, Jamhuri ya Korea Kusin

TANZANIA KUPATA MIKOPO YENYE MASHARTI NAFUU

Serikali ya Jamhuri ya Korea imeiwezesha Tanzania kupata mikopo yenye masharti nafuu kutoka Mfuko wa Ushirikiano wa Maendeleo ya Uchumi (EDCF) wa Korea yenye thamani ya Dola za Marekani bilioni moja ili kugharamia miradi ya maendeleo katika kipindi cha kuanzia mwaka 2021 hadi 2025.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Fedha na Mipango Zanzibar Mhe. Dkt. Saada Mkuya Salum, alieongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano kati ya Korea na Afrika (KOAFEC) kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, alipokutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Uchumi na Fedha wa Korea Mhe. Kyungho Choo, pembezoni mwa Mkutano kati KOAFEC unaoendelea jijini Busan nchini Korea Kusini.

Alisema kuwa mikopo hiyo kutoka Korea imesaidia utekelezaji wa miradi mbalimbali katika pande zote mbili za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na baadhi ya miradi iliyoidhinishiwa fedha mwezi Februari, 2023 ipo katika hatua mbalimbali za maandalizi.

‘‘Miradi iliyokatika hatua mbalimbali za utekelezaji ni pamoja na ujenzi wa hospitali ya rufaa ya Binguni inayotarajiwa kugharimu takriban dola za Marekani milioni 164, kuboresha hospitali ya Taifa ya Muhimbili dola milioni 227.3, ujenzi wa taasisi ya mafunzo dola milioni 75.8 na ujenzi wa taasisi ya teknolojia dola milioni 60, ujenzi wa kituo cha kisasa cha mafunzo ya reli dola milioni 75.8 na fedha nyingine zitaelekezwa katika sekta za nishati, uvuvi na fedha,’’alisema Mhe. Mkuya.

Alisema kuwa Tanzania ilipata mkopo wa masharti nafuu kutoka Mfuko wa Ushirikiano wa Maendeleo ya Uchumi (EDCF) kwa ajili ya ujenzi wa daraja la Selander (Tanzanite Bridge) uliogharimu Dola za Marekani milioni 123.65 ambapo daraja hilo si tu limebadilisha taswira ya jiji la Dar es Salaam, lakini pia limepunguza kwa kiasi kikubwa msongamano wa magari katika barabara ya Ali Hassan Mwinyi.

Aidha, Serikali ya Jamhuri ya Korea kupitia benki ya Exim ya Korea pamoja na Shirika la Bima la Korea (Ksure) imeendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kutekeleza mradi wa reli ya kisasa ya (SGR) ikihusisha utengenezaji wa vichwa na mabehewa ya treni.

‘‘Jumla ya fedha zilizotolewa na benki ya Exim na Ksure kwa ajili ya ununuzi wa vichwa na mabehewa ya treni yanayotengenezwa na Kampuni ya M/S Hyundai Rotem ya Jamhuri ya Korea ni dola za Marekani milioni 302.4”, alieleza Dkt. Mkuya.

Aidha katika mkutano huo, Mhe. Dkt. Mkuya aliiomba Serikali ya Jamhuri ya Korea kuharakisha mradi wa Ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Binguni na mradi wa Uendelezaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kutokana na umuhimu wa miradi hiyo katika kutoa huduma za Afya za kibingwa nchini Tanzania.

Akizungumza kuhusu uchumi wa Tanzania Mhe. Dkt. Mkuya alisema kuwa licha ya changamoto ya Covid 19 na vita ya Urusi na Ukraine Uchumi umeanza kuimarika katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2023 ambapo ukuaji uliorekodiwa ulikuwa wa asilimia 5.6 kwa Bara na ulikuwa asilimia 6.2 kwa Zanzibar.

Mhe. Dkt. Mkuya, aliishukuru Serikali ya Jamhuri ya Korea kwa kuendelea kuiunga mkono Tanzania, kutekeleza ajenda ya Maendeleo ya Taifa kama ilivyoainishwa chini ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2025, Dira ya Maendeleo ya Zanzibar 2050 na Mpango wa Tatu wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2021/22–2025/26 na Mpango wa Maendeleo wa Zanzibar 2021 -2026.

Alisisitiza kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, itaendelea kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Korea kwa ajili ya maendeleo ya watu wetu.

Kwa upande wake Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Uchumi na Fedha wa Korea Mhe. Kyungho Choo, alisema kuwa Korea itaendelea kushirikiana na Tanzania katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Imetolewa na
Kitengo cha Habari na Uhusiano
Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango
05/9/2023

MHE. DKT SAADA MKUYA SALUM AMESHIRIKI KATIKA ZOEZI LA UTOAJI ZAWADI KWA WASHIRIKI KUMI (10)WA ZOEZI LA KILA MWEZI LA “DAI RISITI, SOMBA ZAWADI.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Mhe. Dkt Saada Mkuya Salum leo Sept 04, 2023 ameshiriki katika zoezi la utoaji zawadi Kwa washindi kumi (10) wa zoezi la Kila Mwezi la “Dai Risiti, Somba Zawadi” linaloendeshwa na Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA)

Zoezi hilo limefanyika katika viwanja vya Darajani, Mjini Zanzibar ambapo zawadi mbalimbali zimetolewa ikiwa ni pamoja na Simu, TV, Blenda na Redio Kwa washindi kumi wa Mwezi wa Agosti, 2023

Mhe. Waziri amewataka Wafanyabiashara kudai risiti za kieletroniki pindi wanaponunua bidhaa na kutoa taarifa Kwa Mamlaka ya Mapato Zanzibar Kwa Wafanyabiashara wanaokataa kutoa risiti za kieletroniki.

Nae, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Zanzibar Ndg. Yussuf Juma Mwenda ameeleza kuwa zoezi hilo la utoaji zawadi Kwa wadai risiti bora ni miongoni mwa Mikakati ya kushajihisha Wananchi kudai risiti za kieletroniki pindi wanunuapo bidhaa

“LIPA KODI KWA MAENDELEO YA ZANZIBAR”

Imetolewa na
Kitengo cha Habari na Uhusiano
Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango
04 Sept, 2023

MHE. WAZIRI AMEKUTANA NA MKURUGENZI MKUU WA (USAD) TANZANIA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango, Mhe. Dkt Saada Mkuya Salum Leo Agosti 28, 2023 amekutana na Ujumbe kutoka Shirika la Misaada la Watu wa Marekani (USAID), Ujumbe huo uneongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa USAID Tanzania Mr Craig Hart ambao walifika Ofisini Kwa Mhe. Waziri kujitambulisha

Dkt Saada Mkuya Salum ameutaka Uongozi wa USAID kuendelea kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ikiwa ni pamoja na kuisaidia SMZ katika vipaumbele vyake ambavyo ni elimu, afya, miundombinu, Uchumi wa Buluu, Nishati na kilimo cha kisasa na teknolojia

Imetolewa na
Kitengo cha Habari na Uhusiano
Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango
29 Agosti, 2023

0E6A7570

MHE. WAZIRI AKUTANA NA WAFANYAKAZI WA OFISI YA RAIS, FEDHA NA MIPANGO ZANZIBAR

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Mhe. Dkt Saada Mkuya Salum Leo Agosti 27 amekutana na Wafanyakazi wa Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango pamoja na Taasisi zake

Mkutano huo, umefanyika katika Ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil Kikwajuni, Mjini Zanzibar

Katika Mkutano huo, Mhe. Waziri amewapongeza Wafanyakazi wa Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Kwa kuchangia mafanikio ya Wizara pamoja na Bajeti ya Wizara na Serikali ya Mwaka 2023/2024

Aidha, Mhe. Dkt Saada Mkuya Salum ameeleza kuwa Kuna haja ya kuanzisha Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Rais Fedha na Mipango lenye muundo wa Mwenyekiti, Katibu na Wajumbe Kwa lengo la kufuatilia na kutatua changamoto za Wafanyakazi wa Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango

Katika nasaha zake Mhe. Waziri amewataka Wafanyakazi kutunza vifaa vya Ofisi, kujiepusha na rushwa na ubadhilifu wa mali za Umma pamoja na kujiepusha kutumia intaneti ya Ofisi Kwa masuala binafsi

Nae, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Dkt Juma Malik Akil amewataka Wafanyakazi wa Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango kufanya kazi Kwa bidii, uadilifu na mashirikiano

Pamoja na mambo mengine, Wafanyakazi hao wamepata fursa ya kuulzia masuali, kutoa maoni na mapendekezo mbalimbali na Viongozi wa Ofisi ya Rais Fedha na Mipango wakapata fursa za kutoa ufafanuzi wa masuali yaliyoulizwa

Imetolewa na
Kitengo cha Habari na Uhusiano
Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango
27 Agosti, 2023

DSC_0459

MHE: WAZIRI AFUNGUA VITUO VIWILI VYA PBZ

Waziri wa Nchi – Afisi ya Rais- Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Saada Mkuya Salum leo tarehe 07/08/2023 amezindua tawi la PBZ liliopo Airport na Tunguu.

Dkt. Saada amesema amefurahishwa na hatua zinazochukuliwa na PBZ za kuwasogezea karibu huduma za kifedha wananchi.

Dkt. Saada amesema kituo cha Airport ni kituo pekee ambacho kinatoa huduma zote za kibenki kwa masaa 24 na siku zote za wiki.

Dkt. Saada amefurahishwa kwakua PBZ inafanya mabadiliko makubwa ya kimaendeleo.

Aidha Dkt. Saada amesema kuwa PBZ inafanya vizuri sana na inaelekea kufikia maono ya Mhe. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt Hussein Ali Mwinyi ni kuona maendeleo yapatikana Nchi ikiwemo kuwasogezea karibu huduma za kifedha na kupatikana kwa urahisi Nchini.

Dkt. Saada amesema kuongezeka kwa watumiaji wa huduma za kifedha hii inatokana na dira ya Maendeleo ya 2050, ilani ya CCM ,Sera ya fedha pamoja na Sera ya Uwekezaji Nchini.

Nae Mkurugenzi Mtendaji Dkt. Muusin S. Masoud amesema PBZ inalengo la kuwasogezea wananchi huduma bora za kibenki pia inatoa gawio kwa Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar na matarajio yao kufungua matawi ndani ya Zanziba, Tanzania na Afrika kwa ujumla.

Imeandaliwa na
Kitengo cha habari na Uhusiano
Ofisi ya Rais- Fedha na Mipango