Aidha, katika ziara hiyo Dkt. Saada amegundua kuwa kampuni ya “Fanikisha Limited” ilikuwa inatoa huduma hizo bila ya kuwa na kibali kutoka Ofisi ya Rais – Fedha na Mipango, ambapo ni kunyume kwa mujibu wa Sheria na Miongozo iliyoweka na Ofisi.
Kampuni ya “Fanikisha Limited” inatoza kiwango cha riba ya mikopo cha asilimia kumi na tano (15%) kwa mwezi badala ya kiwango cha asilimia tatu nukta tano (3.5%) kilichowekwa na Ofisi. Hata hivyo, mikopo iliyokuwa inatolewa na Kampuni ya “Fanikisha Limited” ni Mikopo Kaushadamu.
Hivyo, Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Fedha na Mipango Dkt. Saada Mkuya Salum amechukuwa hatua ya kuifungia kampuni “Fanikisha Limited” Kutoa Huduma za Fedha nchini kuanzia tarehe 21 Febrauari, 2024 mpaka itakapokamilisha taratibu za Sheria na Miongozo iliyowekwa na Ofisi ya Rais – Fedha na Mipango.
Aidha, Mhe. Dkt. Saada katika ziara hiyo ameongozana na Kamishna wa Sera za Kodi na Fedha wa Ofisi ya Rais – Fedha na Mipango. Ng. Haji A. Haji
Imeandaliwa na Kitengo cha Habari na Uhusiano Ofisi ya Rais – Fedha na Mipango
Kikao hicho kimejadili agenda mbalimbali za kimaendeleo kikao hicho pia kimepata fursa ya kumuaga aliekuwa Naibu Waziri Mhe. Ali Suleman Ameir ambae amepata uteuzi na kuwa Waziri wa Ofisi ya Rais Ikulu.
Kikao hicho pia kimepata fursa ya kumkaribisha Naibu Waziri Mhe. Juma Makungu Juma na kuendelea kujadili mada mbalimbali zilizowashilishwa katika kikao hizho cha Uongozi wa Ofisi ya Rais – Fedha na Mipango.
Mhe Dkt Saada Mkuya Salum amewataka wanasheria wote wa serikali na makatibu wakuu kuacha kusaini mkataba wowote wenye vipengele vya kodi na baadae kuomba kusamehewa kodi kwani hiyo sio kazi yao kwani msamaha wa kodi unatolewa Ofisi ya Rais – Fedha na Mipango na msamaha unautaratibu wake ambao upo kisheria .
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango, Dk. Saada Mkuya Salum, alieleza hayo wakati akifungua Jukwaa la bajeti la mwaka 2024/2025 kwa serikali kuu liloshirikisha makatibu wakuu katika ukumbi wa Shekh Idrissa Abdul wakil Kikwajuni.
“Tufahamu kuwa kodi inayokusanya ndio sisi inayotulipa mishahara, huduma za afya, elimu na huduma nyengine za barabara, maji, pencheni zinatokana na hii kodi,” alisema.
Hivyo, aliahidi kwamba Ofisi yake itaendelea kulisimamia jambo hilo ili kuona kunakuwa na nidhamu ya ukusanyaji wa mapato ya serikali na kuangalia namna bora ya kuhakikisha kila mmoja anawajibika katika usimamizi wa sheria za kodi nchini.
“Jambo hili tutaendelea kulisisitiza ili kufikia utekelezaji wa bajeti kwa zaidi ya asilimia 100 na jambo hili linawezekana ikiwa kila mmoja wetu atakuwa mlinzi wa kodi ambazo ni fedha za umma,” alisisitiza.
Waziri Saada akizungumzia bajeti zinazotaarishwa kuzingatia masuala ya kijinsia alisema bado kuna muamko mdogo kuhusiana na utayarishaji wa bajeti unaozingatia jinsia hasa kunufaika kwa wanawake katika masuala mbalimbali ikiwemo kilimo, afya na mambo mengine.
Alisema pamoja na kujaribu kujenga uwezo kwa watendaji lakini jambo hilo bado halijafanikiwa hivyo Ofisi yake itahakikisha inaweka nguvu kubwa katika baadhi ya wizara tano ikiwemo Wizara ya Afya, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Wizara ya Elimu, Wizara ya Maji, Nishati na Madini na Wizara ya Uchumi wa Bluu ili kuona namna gani wataweza kutekeleza bajeti zinazozingatia jinsia.
Mbali na hayo Waziri Saada alisema wizara italifanyia kazi eneo la manunuzi na eneo la mapato ili kuhakikisha manunuzi yote yanayofanywa serikalini yanazingatia sheria.
“Mara hii tunakwenda kwenye bajeti ambayo ya uhalisia utaingiziwa fedha na kazi zako utaonesha unazotakiwa uzifanye kisingizio cha kuwa huna pesa hujafanya hicho kitakuwa kimeisha.
Jukwa hilo limehudhuriwa na Viongozi wakuu wa Ofisi ya Rais – Fedha na Mipango.
Aidha, washiriki wa jukwaa hilo walimuomba Mwenyekiti kuzingatia mijadala yao Sambamba na hayo walisisitiza kuomba kuwa miradi ya kimkakati kusimamiwa na serikali kuu na sio Idara au Mashirika ili kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwa wakati.
Jukwaa hilo lipo kwa mujibu wa sheria ya usimamizi wa fedha za umma ambapo mada mbalimbali za uchumi na matumizi ziliwasilishwa na kuzingatia matumizi na makusanyo ya bajeti kwa mwaka 2024/2025.
Waziri wa Nchi-Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Mhe. Dkt Saada Mkuya Salum leo Novemba 5,2023 alikuwa mgeni rasmi katika Kongamano la kuadhimisha miaka mitatu (3) ya Uongozi wa Rais WA Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt Hussein Ali Mwinyi
Kongamano hilo limetayarishwa na Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango pamoja na taasisi zake ambapo wanafunzi wa vyuo vikuu mbali mbali walialikwa katika kongamano hilo, miongoni mwa Vyuo Vikuu vilivyoshiriki ni pamoja na Chuo Kikuu Cha Taifa Cha Zanzibar (SUZA), Chuo Cha Utawala WA Umma(IPA), Chuo Cha Mwalimu Nyerere, Zanzibar University (ZU) pamoja na Al Sumeit Cha Chukwani
Lengo la kongamano hilo ni kuyaelezea Mafanikio ya Miaka mitatu (3) ya Dkt Mwinyi Madarakani
Katika Kongamano hilo Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Dkt. Juma Malik Akil aliwasilisha Ripoti ya utekelezaji ya Miaka mitatu ya Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango na kueleza kuwa Miaka mitatu Dkt Mwinyi Miradi mbalimbali ya Maendeleo imetekelezwa, Miradi ya Skuli, Hospitali, Barbara, Bandari na kuongeza pencheni jamii kutoka 20,000/ Hadi 50,000/ pamoja na nyongeza ya mishahara
Aidha, taasisi za ofisi ya Rais Fedha na Mipango zilipata fursa za kuwasilisha taarifa zao za utekelezaji wa Miaka mitatu, taasisi zilizowasilisha taarifa zao ni Shirika la Bima la Zanzibar, Benkj ya Watu wa Zanzibar (PBZ), Mamlaka ya Manunuzi pamoja na Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA)
Nao, baadhi ya wanafunzi walipata fursa ya kuelezea Mafanikio ya Dkt. Mwinyi, Ali Ahmada kutoka Chuo Kikuu Cha Summeit Chukwani ameipongeza Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Kwa kazi kubwa wanayoifanya kuleta Maendeleo na kuiomba Serikali kuongeza kiwago Cha Fedha za mikopo Kwa wanafunzi WA vyuo vikuu
Aisha Mussa kutoka Chuo Cha Taifa Cha Zanzibar (SUZA) ameitaka Ofisi ya Rais Fedha na Mipango kuwapatia elimu na mafunzo wajasiriamali juu ya matumizi ya Mifumo ya kidigitali katika kazi zao
Imetolewa na Kitengo Cha Habari na Uhusiano Ofisi ya Rais, Fedha na Mioango.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – Fedha na Mipango Mhe. Dkt Saada Mkuya Salum leo Novemba 3,2023 amezindua Bodi ya Wakurugenzi wa Taasisi ya Wahasibu, Wakaguzi na Washauri Elekezi wa Kodi (ZIAAT) katika Ukumbi wa taasisi hiyo uliopo katika jengo la iliyokuwa Ofisi ya Mfuko wa Barabara Maisara Mjini Zanzibar
Mhe. Waziri amewataka wajumbe wa Bodi hiyo wawe wabunifu na wasimamie taasisi Kwa maslahi ya Umma pamoja na kufanya uadilifu katika utekelezaji wa majukumu yao.
Dkt. Saada ameshauri kuwa Bodi ya Wakurugenzi wa (ZIAAT) wapitie vizuri Sheria ya (ZIAAT) na wafanye maboresho ya kuingiza masuala ya miamala ya fedha katika Sheria za kiislam pamoja na mambo mengine
Nae, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Taasisi ya Wahasibu, Wakaguzi na Washauri Elekezi wa Kodi Bw. Juma Amour Mohammed ameeleza kuwa Bodi itafanya kazi Kwa uweledi wa hali ya juu katika kuboresha tasnia ya uhasibu na Ukaguzi pamoja na kutoa elimu Kwa wajumbe wa Bodi ili wafahamu Sheria ya (ZIAAT)
Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Wahasibu, Wakaguzi na Washauri Elekezi wa Kodi CPA. Ame Burhan Shazil ameeleza kuwa taasisi hii imeanzishwa Kwa Sheria No 7 ya Mwaka 2022 malengo yake ni pamoja na kuongeza ubora wa huduma zitolewazo na (ZIAAT), kuwatambua na kuwasajili Wahasibu, Wakaguzi na Washauri Elekezi wa kodi
Katika hafla hiyo, pia alikuwepo Muwakilishi wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi CPA Charles Masabu ambae ameitaka (ZIAAT) kufanya kazi zake kitaalamu zaidi na wakianza tu kuwasajili Wahasibu, Wakaguzi na Washauri Elekezi wa Kodi ni vyema wakasajiliwa Kwa njjia ya kieletroniki na hili litarahisisha ukusanyaji wa Kodi
Imetolewa na Kitengo cha Habari na Uhusiano Ofisi ya Rais, Fedha n Mipango
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais -Fedha na Mipango Mhe. Dkt Saada Mkuya Salum leo Oktoba 26, 2023 amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kifedha (ASA Microfinance Limited) Bibi Karin A. M.Kersten) ambae ameambatana na wajumbe mbalimbali akiwemo Mkurugenzi wa ASA Kwa upande wa Tanzania Ndg Muhammad Shah Newaj
Bibi Kersten ameeleza kuwa Uongozi wa ASA umefika Ofisini Kwa Mhe. Waziri Kwa lengo la kujitambulisha na kueleza kuwa Kwa upande wa Tanzania Ofisi za ASA Microfinance Limited zinapatikana Kinondoni, Jijini Dar es Salaam
Aidha, Bibi Kersten ameendelea kueleza kuwa Kwa upande wa Zanzibar Ofisi za ASA zinapatikana Maungani, Wilaya ya Magharib ‘B’ Mkoa wa Mjini Magharib
Dkt Saada Mkuya ameushukuru Uongozi wa ASA Kwa kufungua tawi lake Kwa upande wa Zanzibar kwani itakuwa ni fursa Kwa wajasiriamali wa sekta mbalimbali hasa sekta ya Uchumi wa Buluu kwani ndio kipaumbele Cha kuwakomboa Wazanzibari wengi ambao wanajishhhulisha na kilimo Cha mwani na uvuvi wa kawaida.
Imetolewa na Kitengo cha Habari na Uhusiano Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Fedha na Mipango Mhe. Dkt Saada Mkuya Salum Leo Oktoba 25, 2023 amemuwakilisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt Hussein Ali Mwinyi katika Uzinduzi wa Airpay Tanzania pamoja na mfumo wa Public Private Partnership (PPP) katika Ukumbi wa Golden Tulip Mjini Zanzibar
Mhe. Saada Mkuya Kwa niaba ya Mhe. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi ameeleza kuwa zana ya Uchumi wa Buluu itafanya kazi vizuri kupitia mfumo wa Airpay kwani itarahisisha miamala ya kifedha Kwa njia za cashless pamoja na kuweza kutambua miamala ya kifedha inayofanywa na wafanyabiashara na wawekezaji wa sekta hiyo.
Mhe. Waziri Saada ameitaka Airpay Tanzania kufanya kazi Kwa karibu na Taasisi za SMZ kama ZRA ili kurahisha ukusanyaji wa Kodi Kwa njia za kieletroniki
Nae, Mkurugenzi Mkuu wa Airpay Mr Kunal Jhunjhunwala ameeleza kuwa lengo la teknolojia hii ni kurahisisha miamala ya kifedha na malipo na Kila mtu aweze kufikiwa na kutumia huduma hii
Aidha, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Serikali Mtandao Zanzibar Ndg Said Seif Said ameeleza kuwa Airpay Tanzania itasaidia Wananchi kupata huduma Kwa njia ya kidigitali pamoja na kuwarahisishia wawekezaji na wafanyabiashara kujisajili na kufanya malipo Kwa urahisi zaidi
Imetolewa na Kitengo cha Habari na Uhusiano Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango
Naibu katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Ndg. Aboud H. Mwinyi leo Oktoba 19, 2023 amefungua warsha ya siku mbili kuhusu mafanikio na changamoto za programu zinazodhaminiwa na UNICEF katika Ukumbi wa Golden Tulip Mjini Zanzibar
Ndg. Aboud ameeleza kuwa, semina hii ni muhimu sana kwani sekta husika ikiwa ni pamoja na maji, afya, elimu pamoja na ustawi wa jamii zimefanikiwa Kwa kiasi kikubwa Kwa mchango wa UNICEF katika kuboresha sekta hizo.
Aidha, Ndg. Aboud amewataka washiriki wa warsha hiyo kupitia Kwa umakini changamoto zilizojitokeza Mwaka uliopita ili zisiwe kikwazo Kwa Mwaka mpya wa utekelezaji wa programu hizo.
Imetolewa na Kitengo cha Habari na Uhusiano Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango
Waziri wa Nchi – Ofisi ya Rais – Fedha na Mipango Mhe Dkt Saada Mkuya Salum leo amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkaazi wa Benki ya Dunia Nchini Tanzania Ndg. Nathan Balete mazungumzo hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Rais – Fedha na Mipango
Mhe Dkt. Saada akiwa na mgemi wake wamejadili kwa pamoja Miradi ya Maendeleo ambayo inafadhiliwa na benki ya Dunia ikiwemo miradi inayoendelea na Miradi ya vipao mbele vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ikiwemo miradi ya kuimarisha Nishati mbadala( ZEST)
Mradi wa kuimarisha miundombinu ya maji Unguja na Pemba, Mradi wa Elimu ambao unatekelezwa kwa pamoja na Tanzania bara mradi huu unalenga kuboresha mazingira ya kusomea kwa vyuo vikuu kwa kujengwa miundombinu mbalimbali
Aidha Dkt. Saada ameishukuru Benki ya Dunia kwa kuendelea kushirikiana na Zanzibar katika kuleta maendeleo ya haraka hapa nchini.
Mhe dkt. Saada amesema Mradi wa sekta ya Afya utasaidia kuboresha vituo vya afya nchini, na kujenga uwezo wa madaktari na madaktari bingwa sambamba na kutatua changamoto za mama wajawazito na watoto wakati wa kujifungua.
Mkurugenzi Nathan atakuwa na ziara ya siku mbili hapa Zanzibar akikagua Miradi iliyofadhiliwa na Benki ya Dunia
Imeandaliwa na Kitengo cha Habari na Uhusiano Ofisi ya Rais – Fedha na Mipango
Serikali ya Jamhuri ya Korea imeiwezesha Tanzania kupata mikopo yenye masharti nafuu kutoka Mfuko wa Ushirikiano wa Maendeleo ya Uchumi (EDCF) wa Korea yenye thamani ya Dola za Marekani bilioni moja ili kugharamia miradi ya maendeleo katika kipindi cha kuanzia mwaka 2021 hadi 2025.
Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Fedha na Mipango Zanzibar Mhe. Dkt. Saada Mkuya Salum, alieongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano kati ya Korea na Afrika (KOAFEC) kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, alipokutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Uchumi na Fedha wa Korea Mhe. Kyungho Choo, pembezoni mwa Mkutano kati KOAFEC unaoendelea jijini Busan nchini Korea Kusini.
Alisema kuwa mikopo hiyo kutoka Korea imesaidia utekelezaji wa miradi mbalimbali katika pande zote mbili za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na baadhi ya miradi iliyoidhinishiwa fedha mwezi Februari, 2023 ipo katika hatua mbalimbali za maandalizi.
‘Miradi iliyokatika hatua mbalimbali za utekelezaji ni pamoja na ujenzi wa hospitali ya rufaa ya Binguni inayotarajiwa kugharimu takriban dola za Marekani milioni 164, kuboresha hospitali ya Taifa ya Muhimbili dola milioni 227.3, ujenzi wa taasisi ya mafunzo dola milioni 75.8 na ujenzi wa taasisi ya teknolojia dola milioni 60, ujenzi wa kituo cha kisasa cha mafunzo ya reli dola milioni 75.8 na fedha nyingine zitaelekezwa katika sekta za nishati, uvuvi na fedha,’’alisema Mhe. Mkuya.
Alisema kuwa Tanzania ilipata mkopo wa masharti nafuu kutoka Mfuko wa Ushirikiano wa Maendeleo ya Uchumi (EDCF) kwa ajili ya ujenzi wa daraja la Selander (Tanzanite Bridge) uliogharimu Dola za Marekani milioni 123.65 ambapo daraja hilo si tu limebadilisha taswira ya jiji la Dar es Salaam, lakini pia limepunguza kwa kiasi kikubwa msongamano wa magari katika barabara ya Ali Hassan Mwinyi.
Aidha, Serikali ya Jamhuri ya Korea kupitia benki ya Exim ya Korea pamoja na Shirika la Bima la Korea (Ksure) imeendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kutekeleza mradi wa reli ya kisasa ya (SGR) ikihusisha utengenezaji wa vichwa na mabehewa ya treni.
‘‘Jumla ya fedha zilizotolewa na benki ya Exim na Ksure kwa ajili ya ununuzi wa vichwa na mabehewa ya treni yanayotengenezwa na Kampuni ya M/S Hyundai Rotem ya Jamhuri ya Korea ni dola za Marekani milioni 302.4”, alieleza Dkt. Mkuya.
Aidha katika mkutano huo, Mhe. Dkt. Mkuya aliiomba Serikali ya Jamhuri ya Korea kuharakisha mradi wa Ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Binguni na mradi wa Uendelezaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kutokana na umuhimu wa miradi hiyo katika kutoa huduma za Afya za kibingwa nchini Tanzania.
Akizungumza kuhusu uchumi wa Tanzania Mhe. Dkt. Mkuya alisema kuwa licha ya changamoto ya Covid 19 na vita ya Urusi na Ukraine Uchumi umeanza kuimarika katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2023 ambapo ukuaji uliorekodiwa ulikuwa wa asilimia 5.6 kwa Bara na ulikuwa asilimia 6.2 kwa Zanzibar.
Mhe. Dkt. Mkuya, aliishukuru Serikali ya Jamhuri ya Korea kwa kuendelea kuiunga mkono Tanzania, kutekeleza ajenda ya Maendeleo ya Taifa kama ilivyoainishwa chini ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2025, Dira ya Maendeleo ya Zanzibar 2050 na Mpango wa Tatu wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2021/22–2025/26 na Mpango wa Maendeleo wa Zanzibar 2021 -2026.
Alisisitiza kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, itaendelea kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Korea kwa ajili ya maendeleo ya watu wetu.
Kwa upande wake Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Uchumi na Fedha wa Korea Mhe. Kyungho Choo, alisema kuwa Korea itaendelea kushirikiana na Tanzania katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.
Imetolewa na Kitengo cha Habari na Uhusiano Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango 16 Sept, 2023