WhatsApp Image 2023-07-18 at 18.16.42

MHE. DKT SAADA MKUYA SALUM ATETA NA VIONGOZI WA BENKI KUU YA TANZANIA TAWI LA ZANZIBAR

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Mhe. Dkt Saada Mkuya Salum leo Julai 18, 2023 amekutana na kufanya mazungumzo na Uongozi wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), tawi la Zanzibar

Hafla hiyo, imefanyika katika Ukumbi wa BOT Kinazini Mjini Zanzibar

Mhe. Waziri ameeleza kuwa lengo la ziara hiyo ni kutaka BOT kuzidi kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kutokana na mabadiliko ya Kiuchumi Zanzibar

Aidha, Mhe. Waziri ameutaka Uongozi wa BOT kuendelea kutoa elimu ya fedha Kwa Umma ili Wananchi waendane na mabadiliko ya teknolojia na mifumo ya fedha

Dkt Saada Mkuya Salum ameendelea kusisitiza Uongozi wa BOT kushirikiana na Serikali katika kuboresha mifumo ya fedha ili kuongeza ufanisi wa ukusanyaji mapato ya Serikali

Nae, Mkurugenzi wa BOT (Tawi la Zanzibar) Dkt Camilius Kombe ameeleza kuwa BOT, tawi la Zanzibar imefanikiwa kupunguza mfumuko wa bei Zanzibar, ambapo Kwa Sasa ni 6.5,%, Burundi mfumuko wa bei 28%, na Rwanda ni 20%, hivyo BOT imefanikiwa Kwa kiasi kikubwa kupunguza mfumuko wa bei.

Dkt Kombe ameendelea kueleza kuwa Sekta ya Fedha Zanzibar imeimarika Kwa kiasi kikubwa kwani Kwa sasa Zanzibar Kuna taasisi za Fedha (Mabenki) 14, Matawi 33, ATM 70 na Mawakala 816

Dkt Camilius amemshukuru Mhe. Waziri Kwa kufanya ziara ya BOT na kumuahidi Mhe. Waziri kuwa maelekezo yote watayafanyia kazi pamoja na kutoa elimu ya fedha Kwa Umma

Imetolewa na
Kitengo cha Habari na Uhusiano
Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango
18 Julai, 2023

Tags: No tags

Comments are closed.