Serikali ya Mapinduzi Zanzibar

wizara ya Fedha na Mipango

 

Waziri wa Fedha na Mipango Mhe.Dkt Juma Malik Akil amewasitiza wastaafu watarajiwa kutumia vizuri mafao ya kustaafu katika uwekezaji sahihi ili kuhimili maisha kipindi cha uzeeni

Ambapo anazitaja kuwa ni jitihada za serikali katika kuwajali wastaafu na kuimarisha mfuko huo ili uendelee kuleta tija katika jamii

Tukio hili linaanza uzinduzi wa kitabu cha safari ya ustaafu ambapo ni dira ya kuwaongoza na kutafakari katika maisha yao baada ya kustaafu

Mara baada ya tukio hilo Dkt Akil anazungumza na wastaafu watarajiwa katika mafunzo ya maandalizi ya kustaafu kwa wastaafu watarajiwa watakaolipwa na mfuko wa hifadhi ya jamii Zanzibar katika ukumbi wa zssf Michenzani Mall anasema wastaafu wawe watulivu wajiandae na maisha mapya baada ya kustaafu kwao

Nae Mkurugenzi Mwendeshaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar Ndg. Nassor Shaaban Ameir anasema mafunzo hayo yataleta chachu ya kuwaondolea hofu wastaafu juu ya matumizi sahihi ya mafao hayo ili kuendelea kujiinua kiuchumi

Nao Wastaafu watarajiwa wamesema watakuwa makini na ushauri juu ya matumizi ya fedha zao za kustaafu

Scroll to Top