Serikali ya Mapinduzi Zanzibar

Ofisi ya Rais Fedha na Mipango

Kitengo cha Habari Mawasiliano na Uhusiano

Kitengo hiki kitahusika na masuala ya mahusiano kati ya Ofisi na taasisi nyengine, kuratibu malalamiko na kuzitangaza shughuli za Ofisi Kitengo hiki kitaongozwa na Mkuu wa Kitengo.

Majukumu ya Kitengo.

  • Kupokea maoni na hoja za wananchi, kuzifuatilia na kutoa taarifa kwa mamlaka husika kwa lengo la kufanyiwa kazi.
  • Kukuza na kujenga uhusiano mwema kati ya Ofisi ya Rais Fedha na Mipango na Taasisi nyengine;
  • Kupokea malalamiko kutoka kwa wadau juu ya utendaji wa Ofisi ya Rais Fedha na Mipango;
  • Kufuatilia maendeleo na changamoto za mahusiano kwa Ofisi ya Rais Fedha na Mipango;
  • Kuweka mazingira mazuri na kukuza mahusiano kazini baina ya watumishi wa Ofisi, watumishi wa Taasisi nyengine na jamii kwa ujumla (afya, michezo, usalama na utamaduni);
  • Kuratibu na kusimamia masuala mbalimbali ya kiitifaki ya Ofisi;
  • Kuratibu na kupokea wageni wa Ofisi ya Rais Fedha na Mipango.
Scroll to Top