Serikali ya Mapinduzi Zanzibar

Ofisi ya Rais Fedha na Mipango

Divisheni ya Uandaaji Bajeti

Divisheni hii inashughulika na uandaaji wa bajeti kwa kuingizwa taarifa za bajeti kwenye mfumo wa kielektronik.

Majukumu ya Divisheni ya Uandaaji Bajeti

  • Kuratibu uwasilishwaji wa bajeti za Mawizara na kusimamia uingizwaji wa taarifa za bajeti kwenye mfumo wa kielectroniki;
  • Kusimamia uchapishaji wa hutuba ya bajeti ya Serikali pamoja na makadirio ya Mapato na matumizi;
  • Kuratibu mswada wa fedha na matumizi;
  • Kuratibu utekelezaji wa Bajeti kwa kushirikiana na Ofisi ya Mhasibu Mkuu/ Hazina, Idara ya fedha za nje na Tume ya Mipango;
  • Kubuni njia bora za kuandaa mijadala ya kibajeti inayohusiana na Mapato na matumizi kwa Wizara na Taasisi za Serikali;
  • Kubuni makadirio na makisio ya Mapato na matumizi ya Serikali kwa Wizara na Taasisi za Serikali;
  • Kusimamia muongozo wa utayarishaji wabajeti;
  • Kuwasilisha nyaraka za bajeti kwa Makatibu Wakuu, Baraza la Mapinduzi (BLM) na Baraza la Wawakilishi (BLW);
  • Kubuni mipango kazi wa Idara kwa mashirikiano na divisheni nyengine;
  • Kuandaa ripoti za utekelezaji wa kazi ikiwemo ripoti ya robo, nusu na mwaka.
Scroll to Top