Serikali ya Mapinduzi Zanzibar

Ofisi ya Rais Fedha na Mipango

Divisheni ya Fedha na Deni La Taifa

Divisheni ya fedha na deni la Taifa inashughulika na udhibiti na usimamizi wa deni la Taifa.

Majukumu ya Divisheni ya Fedha na Deni la Taifa

  • Kusimamia Deni la Taifa kwa kuandaa muundo wa usimamizi wa deni na kuhakikisha mzigo wa madeni unadhibitiwa.
  • Kutathmini mapendekezo ya mikopo ya ndani na nje na kuandaa usimamizi wa kujitegemea katika wajibu wa kifedha wa Serikali.
  • Kudumisha “database” ya usimamizi wa madeni ya mikopo na dhamana ya Serikali.
  • Kuandaa ripoti za madeni kama zilivyoainishwa katika Sheria ya Usimamizi wa Fedha za Umma.
  • Kusawazisha taarifa za madeni ya Serikali na wanaotudai, BOT, Wizara ya Fedha na Mipango, SMT na wadau wengineo.
  • Kukusanya, kuhakiki na kutoa taarifa ya madeni yote ya ndani ya Serikali.
  • Kutayarisha makisio ya riba ya Deni la Umma na malipo ya Kima kwa ajili ya kuiingiza katika bajeti ya mwanzo.  
  • Kutimiza matakwa ya Serikali kifedha na kuweka gharama ndogo na madeni kadiri iwezekavo zinazohusiana na vihatarishi.
  • Kutunza kumbukumbu za Madeni ya Serikali na kufuatilia mfumo wa Usimamizi wa madeni.
  • Kutoa dhamana na kuweka kumbukumbu za malipo ya dharura kwa Taasisi za Umma, mashirika na Serikali za mitaa.
  • Kutoa taarifa za mwenendo wa Fedha katika Mfuko Mkuu, malipo ya deni na salio la mtawanyo wa mkopo.
  • Kutoa kazi za sekriterieti ya Kamati ya Usimamizi wa Deni la Zanzibar.
Scroll to Top