WhatsApp Image 2023-07-15 at 17.16.41 (1)

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Mhe. Dkt Saada Mkuya Salum Leo Julai 15, 2023 amefanya ziara ya kutembelea vituo vya kupokelea Pencheni jamii ya Wazee kuanzia Miaka 70

Zoezi la kuwalipa Wazee hao limeanza leo Julai 15,2023 katika Wilaya za Mahgarib ‘A’ na Magharib ‘B’ Mkoa wa Mjini Magharib

Mhe. Waziri, Dkt Saada Mkuya Salum ameeleza kuwa awali Pencheni Jamii ilikuwa ni elfu ishirini (20,000) lakini kutokana na Agizo la Mhe. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe Dkt Hussein Ali Mwinyi kuwa ifikapo Mwaka mpya wa Fedha 2023/2024 kuwa Pencheni Jamii ilipwe elfu khamsini (50,000) Kwa Kila Mzee

Aidha, Dkt Saada ameongeza kuwa wakati Wazee wanalipwa Pencheni jamii elfu ishirini (20) Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilikuwa inatumia Milioni mia SITA (600) Kwa Mwezi lakini Kwa Sasa ambapo Kuna ongezeko la Malipo ya Pencheni Jamii kutoka Tsh 20,000/ Hadi 50,000/ Serikali inatumia Bilioni Moja na Milioni Mia Nne Kwa Mwezi.

Mhe. Waziri amewashukuru Viongozi na Watendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ), Wizara ya Ustawi wa Jamii pamoja Masheha Kwa mashirikiano yao mazuri licha ya changamoto ndogo ndogo zilizojitokeza

Wazee waliofika kupokea Pencheni jamii wameelezea furaha yao ya ongezeko la Pencheni Jamii kutoka 20,000/ Hadi 50,000/ na kumpongeza Mhe. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt Hussein Ali Mwinyi Kwa kuwajali na kuwaongezea Pencheni Jamii ili fedha hizo ziwasaidie katika Maisha yao.

Imetolewa na
Kitengo cha Habari na Uhusiano
Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango
15 Julai,2023