WhatsApp Image 2024-05-03 at 17.42.26_78525633

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetiliana saini na kampuni ya CRJE juu ya Mkataba wa Ujenzi Mradi wa Uimarishaji wa Miji Kwa Upande wa Unguja.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar leo tarehe 2/05/2024 imetiliana saini na kampuni ya CRJE juu ya Mkataba wa Ujenzi Mradi wa Uimarishaji wa Miji Kwa Upande wa Unguja.

Kwa niaba ya Serikali Mkataba huo umewekwa saini na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Fedha na Mipango Dkt. Juma Malik Akil ambapo jumla Bilioni 40,535,043,304.24 zinatarajiwa kutumika kwa ujenzi wa maeneo ya Sebleni – Kwa Wazee, Meya- Magomeni na Mtaro wa Mfumo C, kwa upande wa CRJE mkaba huo umesainiwa na XU Chang ambae ni Meneja wa kampuni.

Mradi huo utaipa hadhi na kuyakuza maeneo ya Mjini kwa i ) kujenga na kukarabati Mitaro ya mvua yenye urefu wa kilomita 4.76
ii) kuimarisha Maeneo ya Wazi kwa kufanya uboreshaji wa viwanja 3 vya mpira viliopo katika eneo la Sebleni Kwa Wazee

iii) Ujenzi wa barabara za ndani zenye urefu wa kilomita 9.14 na uwekaji wa taa zinazotumia nguvu za jua.

iv) kujenga soko moja la wajasiriamali katika eneo la Meya.

Aidha Katibu Mkuu ameweka saini kupitia Mradi wa Ukuzaji Uchumi Jumuishi Zanzibar ( BIG – Z) ambapo ni Mradi unaofadhiliwa na Benki ya Dunia.

Mradi utatekelezwa kwa miezi 30 Sawa na miaka 2 na nusu kuanzia tarehe ya leo.

Imeandaliwa na
Kitengo cha Habari na Uhusiano
Ofisi ya Rais – Fedha na Mipango

katibu2

Katibu Mkuu Dkt. Juma Malik Akil leo akutana na Ujumbe kutoka Chuo cha Ulinzi cha Taifa (NDC)

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Fedha na Mipango Dkt. Juma Malik Akil leo tarehe 30/04/2024 amekutana na Ujumbe kutoka Chuo cha Ulinzi cha Taifa (NDC) ambao wapo Zanzibar kwa ziara ya kimasomo. Katibu Mkuu Dkt. Juma amesema ziara hii ina mwanya wa kiuchumi na kiutamaduni na Zanzibar inaendelea kujenga miundo mbinu wezeshi kwa uchumi wa buluu. Dkt. Juma amesema Ujio huu ni kundi la 12 kuja kuitembelea Sekta ya Fedha ambayo ni sekta muhimu inayosimamia Uchumi wa Nchi. Ujumbe huo unajumuisha wanafunzi wa Nchi 15 za Dunia ikiwemo Tanzania. Aidha, Ofisi ya Rais- Fedha na Mipango imepata nafasi ya kuelezea kazi inazozifanya kupitia Taasisi zake ikiwemo Tume ya Mipango, PBZ, ZRA, TRA, ZIAT na Ofisi ya TR. Ujumbe huo umeongozwa na Mkuu wa Chuo Cha Ulinzi cha Taifa Balozi Meja Generali Wilbert Augustine Ibuge. kikao hicho kimefanyika katika Ukumbi wa Bima wa Zanzibar(ZIC).

WhatsApp Image 2023-07-15 at 17.16.41 (1)

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Mhe. Dkt Saada Mkuya Salum Leo Julai 15, 2023 amefanya ziara ya kutembelea vituo vya kupokelea Pencheni jamii ya Wazee kuanzia Miaka 70

Zoezi la kuwalipa Wazee hao limeanza leo Julai 15,2023 katika Wilaya za Mahgarib ‘A’ na Magharib ‘B’ Mkoa wa Mjini Magharib

Mhe. Waziri, Dkt Saada Mkuya Salum ameeleza kuwa awali Pencheni Jamii ilikuwa ni elfu ishirini (20,000) lakini kutokana na Agizo la Mhe. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe Dkt Hussein Ali Mwinyi kuwa ifikapo Mwaka mpya wa Fedha 2023/2024 kuwa Pencheni Jamii ilipwe elfu khamsini (50,000) Kwa Kila Mzee

Aidha, Dkt Saada ameongeza kuwa wakati Wazee wanalipwa Pencheni jamii elfu ishirini (20) Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilikuwa inatumia Milioni mia SITA (600) Kwa Mwezi lakini Kwa Sasa ambapo Kuna ongezeko la Malipo ya Pencheni Jamii kutoka Tsh 20,000/ Hadi 50,000/ Serikali inatumia Bilioni Moja na Milioni Mia Nne Kwa Mwezi.

Mhe. Waziri amewashukuru Viongozi na Watendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ), Wizara ya Ustawi wa Jamii pamoja Masheha Kwa mashirikiano yao mazuri licha ya changamoto ndogo ndogo zilizojitokeza

Wazee waliofika kupokea Pencheni jamii wameelezea furaha yao ya ongezeko la Pencheni Jamii kutoka 20,000/ Hadi 50,000/ na kumpongeza Mhe. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt Hussein Ali Mwinyi Kwa kuwajali na kuwaongezea Pencheni Jamii ili fedha hizo ziwasaidie katika Maisha yao.

Imetolewa na
Kitengo cha Habari na Uhusiano
Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango
15 Julai,2023